Posts

Mambo ambayo Mwanamke hawezi kuyaweka wazi katika Mahusiano

Image
Unapoanzisha mahusaino na mwanamke yeyote yale fahamu fika yapo baadhi yavitu hawezikukkwambia na baadhi ya mambo hayo ni; 1. Idadi ya wapenzi wake wa zamani Wanaume wengi hupenda kujua wao ni wangapi kuwa na mwanamke Fulani. Lakini mwanamke kamwe hawezi akakwambia wewe ni wa ngapi. Kumuuliza jambo hili kunamkera sana mwanamke na ndio maana mara nyingi hawezi akakwambia ukweli. 2. Anakulinganisha na mpenzi wa zamani Mwanamke mara nyingi anakulinganisha na mpenzi wake wa zamani japokuwa hawezi kukwambia waziwazi. Wakati mwingine tabia hii huwafanya wanawake kuwatamani wapenzi wa zamani na hata kurudiana nao endapo watakosa mtu aliye bora kuliko mpenzi wake wa zamani. 3. Kasoro zako Mwanamke kamwe hawezi kukwambia kasoro zako. Wanawake wanajua kumfichiaa mpenzi wao mambo wasiyotaka yajulikane kwa wengine na kwa mpenzi wake. Wanajua njia za kiujanja za kutumia ili kufichua siri zako zote. Mwanamke hawezi kukwambia kasoro zako kwa kuogopa kukuumiza. 4. Mapungufu yake Mwanamke hawezi kukw...

Mama kuwa makini House Girl Yaweza Kuwa Mke Mwenzio

Image
                                    HI  vi ni vibaya House girl kuolewa na baba mwenye nyumba? Ndugu msomaji wa SINIA LA BAHARI Blog.karibu kwenye makala hii maalumu, nimeamua kuandika habari hii ili kujaribu kupunguza mifarakano kwenye familia zetu especially familia zenye wafanyakazi wa ndani wanaojulikana kama house girl. Katika mada hii nimekuwa nikikutana na maswali mengi sana ambayo mda mwingine yalikuwa yakituchanganya hata sisi wenyewe katika kuwajibu wahusika, maswali haya malanyingi yalikuwa yakiulizwa na akina mama. Na kwa upande wa akina baba maswali yao sio mengi ukilinganisha na akina mama, sasa napenda nianze kwa kusema mambo yafuatayo ili wote twende sawa. WAJIBU WA MWANAUME KATIKA FAMILIA:   Mwanaume anawajibu wa kutimiza mahitaji yote ya msingi katika familia yake, moja ya majukumu hayo ni pamoja na kutoa pesa za matunzo ya familia yake kadri ipasavyo, kuonyesha upend...

Maghorofa ya Lugumi kupigwa mnada kwa mara nyingine

Image
Dar es Salaam.Kampuni ya Udalali ya Yono imesema itapiga mnada kwa mara ya pili nyumba za kifahari za mfanyabiashara Saidi Lugumi baada ya ule wa kwanza uliofanyika Septemba 7 kukwama. Mkurugenzi mtendaji wa kampuni hiyo, Scholastica Kevela amewaeleza waandishi wa habari leo Jumatatu kuwa lengo la mnada huo ni kufidia Sh 14 bilioni anazodaiwa Lugumi. "Sio kweli nyumba hizi zimedoda ila thamani halisi katika mnada wa kwanza haukufikiwa na ndio maana tunarudia tena Novemba 9," amesema Kevela. Amesema baada ya mnada wa awali kukwama walirudi kujipanga na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imewapa maelekezo mengine ikiwamo thamani ya nyumba hizo. Soma: Wateja hawajajitokeza kununua mali za Lugumi "Wale wanaotaka majumba haya ya Lugumi waje siku hiyo na tayari Serikali kupitia TRA imetupa maelekezo mapya hasa thamani ya majumba hayo imepanda kuliko ya awali ilivyokuwa," ameongeza Mkurugenzi huyo amesema nyumba hizo zitakazopigwa mnada ziko Mbweni JKT nyumba mbili na  nyu...

Familia ya Lissu yafunguka haya

Image
TUNDU LISSU AKIWA HOSPITALI YA NAIROBI. Familia ya Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu imesema ataendelea kupata matibabu kwenye Hospitali ya Nairobi, Kenya wakati taratibu za kumhamisha zikiendelea. Aidha, familia hiyo imesema itaweka wazi kwa umma siku itakapomhamishia hospitali nyingine mtaalamu huyo wa sheria. Akizungumza na Nipashe kwa simu jana, kaka wa Lissu, Vicent Lissu, alisema mbunge huyo atahamishwa kutoka katika hospitali hiyo kwenda kupata matibabu ya kibingwa zaidi kama ilivyoelezwa Jumanne iliyopita na Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe. "Mheshimiwa Lissu bado anaendelea na matibabu kwenye hospitali ileile," Vicent alisema, "akihamishwa mtajua maana tutaeleza ila kwa sasa bado ni mapema kusema atakwenda nchi gani, itoshe kujua bado yupo Nairobi." Alipoulizwa kuhusu gharama za matibabu ya mbunge huyo na kama kuna deni lolote katika Hospitali ya Nairobi, Vicent alisema: "Hilo ni suala binafsi sana na ...

Mwili wa mtoto wa miaka 3 aliyefukuzwa nyumbani usiku wapatikana

Image
Maafisa waliokuwa wakimtafuta mtoto Sherin Polisi huko Texas wanasema kuwa wamepata mwili wa mtoto wa miaka mitatu Sherin Mathews ambaye alitoweka tarehe 7 mwezi huu, wakati babake alimfukuza kutoka nyumbani kwao mwenda saa tatu usiku kama njia ya kumuadhibu. Polisi waliwaambia waandishi wa habari kuwa mwili huo ulionekana kuwa wa Sherin ambaye habari za kutoweka kwake zilisambaa mjini Dallas na India. Wanandoa hao kutoka India walimpangisha mtoto huyo miaka miwli iliyopita kutoka makao ya kuwatunza watoto nchini India. Mwili huo ulipatikana kwenye andaki kuribu nusu maili kutokan nyumbani kwao siku ya Jumamosi. Babake Sherif, Wesley Mathews alikamatwa na kuachiliwa kwa dhamana, kwa kuhatarisha maisha ya mtoto huyo baada ya kumfukuza kutoka nyumbani usiku kutokana na sababu kuwa alikataa kumaliza maziwa aliyokuwa akinywa. Mamake anasemakana kuwa alikua akilala wakati kisa hicho kilitokea. Wanandoa hao wana mtoto mwingine wa miaka minne ambaye alichukuliwa kutunzwa baada ya kisa hicho

RC Makonda apinga Bomoabomoa ya karne Dsm

Image
Ndugu Zangu Wananchi wa Mkoa wa Dar es Salaam, Naomba kuwatoa hofu, Mimi Paul Makonda nikiwa Mkuu wenu wa Mkoa na mtumishi wa serikali ya awamu ya tano, Napenda kuwataarifu kwamba serikali hii inayoongozwa na Mhe Rais, Dkt. John Pombe Magufuli HAIVUNJI Nyumba ya mtu Bali inaendelea kurasimisha Makazi kama ambavyo ilifanya kimara kwa kuwapatia Hati elfu Sita (6000) kwa Wananchi waliokuwa wamejenga kwenye makazi yasiyo rasmi, jitihada zinaendelea na ndivyo itakayofanyika tarehe 27/10/2017 kwa Wananchi waliojenga katika maeneo ya makongo juu. Naomba niseme, na kama nimemuelewa vizuri alichokisema _Mhe William Lukuvi_ ambae ni Waziri wa Ardhi, Nyumba na maendeleo ya Makazi ni kuwa wananchi wasiendelee kujenga bila vibali vya ujenzi jambo ambalo linawanyima haki yao ya kukopeshwa, kulipa kodi ya majengo, na mwishoni kuwa na miji isiyopangwa vizuri. Naomba kukiri kuwa apo awali kulikuwa na changamoto ya upatikanaji wa vibali vya ujenzi jambo ambalo haliwezi kuwa Adhabu kwa Wan...

Breaking: Lulu akutwa na kesi ya kujibu kuhusu kifo cha kanumba

Image
Mahakama kuu ya Tanzania kanda ya Dar es Salaam leo Oktoba 23, 2017 imemkuta Msanii maarufu wa filamu nchini, Elizabeth Michael Maarufu kama Lulu, anakesi ya Kujibu. Ni kuhusu tuhuma zinazomkabili za kumuua msanii mwenzake, marehemu Steven Kanumba ambaye pia alikuwa ni mpenzi wake, April 6 mwaka 2012. Hatua hiyo imekuja baada ya upande wa Jamhuri kufunga ushahidi wao kwa kuita mashahidi wanne. Kesi imeahirishwa hadi saa tano kamili ambapo Lulu ataanza kujitetea