Posts

Chimbuko la Illuminati na dhana kuhusu nguvu zao

Image
Haki miliki ya picha ALAMY Image caption Baadhi huamini michoro iliyo kwenye dola za Marekani ina uhusiano na Illuminati Ni simulizi ya ulaji njama ambayo bila shaka imevuma zaidi kushinda njama nyingine zote. Ni wachache sana ambao hawajawahi kusikia kuwahusu Illuminati. Huaminika kuwa kundi maalum la watu ambao hudhibiti masuala na uongozi wa dunia, na inasadikika kuwa hufanya shughuli zao kisiri kudhibiti kila kitu na kuunda Utawala Mpya wa Dunia. Kwa wengine, wamehusishwa na utajiri wa ghafla ambao si wa kawaida. Ukitajirika haraka, kunao bila shaka watakaodai kwamba umejiunga na Illuminati. Je, kuna ukweli wowote kuhusu wasiwasi huu? Kuna kundi la watu wanaofanya vikao vya siri kupanga njama za kuitawala dunia na pia kjifaidi wenyewe kwa pesa na utajiri? Simulizi hizi na umaarufu wa illuminati zina ukweli wowote? Wasiwasi huu kuhusu kundi linalopanga njama ya kuweka utawala mpya duniani ulianza miaka ya 1960, sana kutokana na ubunifu wa watu fulani. Kuenea kwa habar...

Utafiti: Wanaume hulemewa na mafua zaidi ya wanawake

Image
Haki miliki ya picha AGES Utafiti mpya unaashiria kwamba ni kweli wanaume hutatizwa na mafua zaidi ya wanawake, jambo ambalo limesababisha kuwepo kwa dhana kwamba huwa kuna mafua ya wanaume. Watafiti nchini Canada wanasema wamepata ushahidi kwamba wanaume hutatizwa zaidi ya mafua ya kawaida na si kwamba huwa wanajifanya kwamba wamezidiwa. Mtafiti mkuu Dkt Kyle Sue amesema wanaume huenda wana mfumo dhaifu kidogo wa kinga mwilini dhidi ya virusi vinavyosababisha mafua wakilinganishwa na wanawake. Hilo huenda likawa huchangia kulemewa kwao na dalili za mafua kuliko wanawake. Je, vitamin D inaweza kuzuia mafua? Kinga mpya ya mwili kushambulia 99% ya HIV Matatizo ya usingizi yaongezeka miongoni mwa watoto Dkt Sue anadokeza kwamba wakati umefika pengine kwa wanaume "kutengewa au kutengenezewa maeneo mahsusi, yaliyo na televisheni na viti vizuri, ambapo wanaweza kuuguza mafua yao hadi wapate nafuu bila usumbufu." Matokeo ya utafiti huo huenda yakafurahiwa sana na wan...

Kutafuta viumbe anga za juu: Sayari hii ndogo inapita na siri kutoka mbali?

Image
Haki miliki ya picha ESO Image caption Mchoro wa Oumuamua Wataalamu wanaofanya kazi katika mradi unaotafuta iwapo kuna dalili za kuwepo kwa viumbe anga za juu wanajiandaa kuchunguza sayari ndogo inayopita katika mfumo wetu wa jua kubaini iwapo kuna uwezekano wa viumbe kama hao kuwepo. Sayari hiyo ndogo yenye umbo ambalo si kawaida kwa sayari iligunduliwa ikielekea kwenye mfumo wa jua siku ya Jumapili 19 Oktoba. Ndiyo sayari ya kwanza kutoka kwa mfumo mmoja wa nyota iliyoingia kwenye mfumo mwingine wa nyota ambayo imetambuliwa kufikia sasa. Sifa zake zinaonesha kwamba imetoka kwenye mfumo wa nyota nyingine. Mpango huo ambao unaungwa mkono na bilionea Yuri Milner utatumia tadubini inayotumia miali ya redio kujaribu kupata mawasiliano kutoka kwa sayari ndogo hiyo Juhudi za kundi hilo la wataalamu zitaanza leo Jumatano, ambapo wataalamu wa anga za juu wataitazama sayari ndogo hiyo, ambayo kwa sasa inasonga kwa kasi kuupita mfumo wetu wa jua. Sayari ndogo hiyo itafuatiliwa kw...

Kwa nini mji wa Jerusalem ni mtakatifu?

Image
Haki miliki ya picha AFP Image caption Maeneo matakatifu ya kidini Jerusalem Kumekuwa na mzozo wa muda mrefu kuhusu udhibiti wa mji wa Jerusalem kati ya Waisraeli na Wapalestina. Mji huo kwa sasa huwa umegawanywa mara mbili, Jerusalem Mashariki na Jerusalem Magharibi. Jerusalem ya Magharibi hutazamwa na Israel kama mji wake mkuu nayo Jerusalem Mashariki hutazamwa kuwa mji mkuu wa taifa la Wapalestina (litakapoundwa), ingawa eneo hilo bado kwa kiwango kikubwa limetawaliwa na Israel tangu vita vya 1967. Tangu wakati wa vita hivyo, Israel imejengwa nyumba za walowezi wa Kiyahudi takriban 200,000 ambao huishi Jerusalem Mashariki, hatua iliyoshutumiwa na jamii ya kimataifa. Eneo hilo huishi Wapalestina takriban 370,000. Israel ilitangaza 1980 Jerusalem yote kuwa mji wake mkuu wa milele, lakini nchi nyingi duniani hazikubali azimio hilo. Hivyo basi, balozi za nchi za kigeni katika Israel ziko nje ya Jerusalem, katika mji wa Tel Aviv. Mzozo huo umefufuliwa tena kutokana na hatu...