Mwanamke ajioa nchini Italia


Laura Mesi, who married herself, cuts her wedding cake
Haki miliki ya picha MARTINI
Image captionFuraha yangu haitegemei uwepo wa mwanamume

Mwanamke moja nchini Italia amejioa yeye mwenyewe kwenye sherehe iliyokuwa na vazi kamili la harusi, keki na wageni 70.
"Ninaamini kuwa kila mmoja wetu ni lazima ajipende," alisema Luara Mesi mwenye miaka 40
Wanaounga mkono ndoa kama hizo wanasema kuwa suala kuu ni kujipenda.
Laura anasema kuwa suala la kujioa lilimkujia miaka miwili iliyopita, baada ya miak 12 ya kuwa kwenye uhusiano wa kimapenzi.

Laura Mesi and her bridesmaidsHaki miliki ya pichaMICAELA MARTINI
Image captionNdoa ya Bi Mesi

"Niliwaambia marafiki zangu na familia kuwa sijapata mpenzi na nikiwa na umri wa miaka 40 nitajioa." aliliambia gazeti la La Repubblica.
"Ikiwa siku moja nitapata mwanamume ambaye nitapanga kuishi naye nitafurahi, lakini furaha yangu haimtegemei yeye."
Bi Mesi anasema kuwa yeye ndiye mwanamke wa Kwanza nchini Italia kufanya harusi ya mtu mmoja.

Carved watermelon at the solo wedding of Laura MesiHaki miliki ya pichaMICAELA MARTINI
Image captionTunda la kusherehekea ndoa ya Laura Mesi

Kati ya maoni yaliyowekwa kwenye picha za Bi Mesi ni pamoja na , "vibaya sana", "umechanganyikiwa" na "kuna tatizo na ubongo wako."
Hata hivyo Bi Mesi ametupilia mbali maoni hayo akisema hakuna mtu atazima tabasamu lake.

Comments

Popular posts from this blog

SAIKOLOJIA : PATA KUFAHAMU MAKUNDI MANNE YA TABIA ZA BINADAMU.

Rapa B.o.B ataka kuthibitisha iwapo dunia ni duara

Kanuni za kuishi na Watu / Binadam Vizuri