Wabunge watwangana makonde Uganda

UgandaHaki miliki ya pichaREUTERS
Image captionWabunge nchini Uganda wamepigana ndani ya ukumbi wa bunge
Wabunge nchini Uganda wamepigana ndani ya ukumbi wa bunge wakiwa katika siku ya pili ya kikao cha kujadili wa muswada wa kuondoa ukomo wa miaka ya kugombea nafasi ya urais kwa mjibu wa katiba ya taifa hilo.
Katika ugomvi huo wabunge hao walirushiana viti, kuharibu vipaza sauti na katika kikao hicho kilichoongozwa na Spika wa bunge, Bi.Rebecca Kadaga.
UgandaHaki miliki ya pichaREUTERS
Image captionWabunge watwangana makonde ukumbini
UgandaHaki miliki ya pichaREUTERS
Image captionWabunge wapambana
Ugomvi huo ulianza pale Spika alipochukua hatua ya kuwafukuza wabunge wapatao 25 wengi wao wakiwa ni wale wa upinzani kwa madai ya utovu wa nidhamu pamoja na waziri wa serikali aliyeshtakiwa kwa kufyatua risasi bungeni siku ya jumanne.
Wabunge hawa wanadai kuwa kama kikomo cha umri wa miaka 75 kitaondolewa basi rais aliyepo kwa sasa atapata mwanya wa kugombea tena mwaka 2021

Comments

Popular posts from this blog

SAIKOLOJIA : PATA KUFAHAMU MAKUNDI MANNE YA TABIA ZA BINADAMU.

Rapa B.o.B ataka kuthibitisha iwapo dunia ni duara

Kanuni za kuishi na Watu / Binadam Vizuri