Utafiti: Wanaume hulemewa na mafua zaidi ya wanawake
Haki miliki ya picha AGES Utafiti mpya unaashiria kwamba ni kweli wanaume hutatizwa na mafua zaidi ya wanawake, jambo ambalo limesababisha kuwepo kwa dhana kwamba huwa kuna mafua ya wanaume. Watafiti nchini Canada wanasema wamepata ushahidi kwamba wanaume hutatizwa zaidi ya mafua ya kawaida na si kwamba huwa wanajifanya kwamba wamezidiwa. Mtafiti mkuu Dkt Kyle Sue amesema wanaume huenda wana mfumo dhaifu kidogo wa kinga mwilini dhidi ya virusi vinavyosababisha mafua wakilinganishwa na wanawake. Hilo huenda likawa huchangia kulemewa kwao na dalili za mafua kuliko wanawake. Je, vitamin D inaweza kuzuia mafua? Kinga mpya ya mwili kushambulia 99% ya HIV Matatizo ya usingizi yaongezeka miongoni mwa watoto Dkt Sue anadokeza kwamba wakati umefika pengine kwa wanaume "kutengewa au kutengenezewa maeneo mahsusi, yaliyo na televisheni na viti vizuri, ambapo wanaweza kuuguza mafua yao hadi wapate nafuu bila usumbufu." Matokeo ya utafiti huo huenda yakafurahiwa sana na wan...






























































Comments
Post a Comment