NI JUU YANGU MIMI KUCHAGUA


Nanyi kama mkiona ni vibaya kumtumikia BWANA, chagueni hivi leo
mtakayemtumikia;... lakini mimi na nyumba yangu tutamtumikia BWANA. Yoshua
24:15.


Katika dunia yetu hii kuna makundi mawili. Moja ni la wale wanaomtazama Mwokozi
wao aliyesulibiwa na kufufuka. Jingine ni la wale wote ambao wamechagua
kutokuutazama msalaba, na kufuata maongozi ya vishawishi vyake Shetani. Kundi hili la
mwisho hujishughulisha sana na uwekaji wa vikwazo mbele ya watu wa Mungu, ili
kusababisha kuanguka kwao, na kuiacha njia ile ya utii na kuingia katika njia pana ya
uasi na mauti....
Wengi huchagua dhambi kwa sababu Shetani anaionyesha kwa namna ambayo
inaonekana kuwa inapendeza kwa wale wasiojilinda na hila zake. Naye anaifanya kazi
yake kwa njia ya pekee kupitia kwa wanaume na wanawake wasiokuwa na maisha safi
ambao hujidai kuwa wao ni watoto wa Mungu. Kwa njia fulani au nyingineyo adui huyo
atatafuta namna ya kuwadanganya wote, yamkini hata walio wateule. Ni pale tu
tunapokuwa washiriki wa tabia ya uungu tunapoweza kuviepuka vishawishi viletavyo
uharibifu ambavyo huletwa kwetu na yule adui wa roho zetu.
Shetani anapotafuta namna ya kuvivunjilia mbali vizuizi vya roho zetu, kwa kutujaribu
ili tujifurahishe katika dhambi, yatupasa kuuhifadhi uhusiano wetu na Mungu kwa imani
iliyo hai, pamoja na kuwa na tumaini katika nguvu zake ziwezazo kutuwezesha sisi
kulishinda kila shambulio linalotusonga. Yatupasa kuukimbia uovu, na kutafuta haki,
upole, na utakatifu.
Wakati umefika kwa kila mmoja wetu kuamua ni upande wa nani tumesimama.
Mawakala wa Shetani watafanya kazi na kila moyo utakaokubali kushughulikiwa naye.
Walakini wapo pia wajumbe wa mbinguni wanaongojea kuwaletea mionzi inayong'aa ya
utukufu wa Mungu wale wote wanaopenda kumpokea. ----- MS 43, 1908.
Ni juu yetu sisi kuchagua iwapo tutahesabiwa pamoja na watumishi wake Kristo au
pamoja na watumishi wake Shetani. Kila siku tunaonyesha kwa tabia yetu tumechagua
kumtumikia nani....
Mpendwa msomaji kijana, umefanya uchaguzi gani? Kumbukumbu ya maisha yako ya
kila siku ikoje? ----- YI, Nov.21, 1883

Comments

Popular posts from this blog

Kanuni za kuishi na Watu / Binadam Vizuri

SAIKOLOJIA : PATA KUFAHAMU MAKUNDI MANNE YA TABIA ZA BINADAMU.

Chanzo cha saratani ya matiti