UPENDO UKAJENGA DARAJA


Hili ndilo pendo, si kwamba sisi tulimpenda Mungu, bali kwamba Yeye alitupenda sisi,
akamtuma Mwanawe kuwa kipatanisho kwa dhambi zetu. 1 Yohana 4:10.

Upendo wa Mungu kwa ulimwengu huu haukudhihirishwa kwa sababu ya kumtuma
Mwanawe, bali kwa sababu aliupenda ulimwengu huu ndio maana alimtuma Mwanawe
ulimwenguni ili Uungu uliovikwa ubinadamu upate kuugusa ubinadamu, wakati Uungu
Wake unashikamana na Mungu. Japokuwa dhambi ilikuwa imefanya shimo kubwa kati
ya mwanadamu na Mungu wake, wema wake Mungu uliweka mpango wa kujenga daraja
juu ya shimo hilo kubwa. Je! alitumia vifaa gani? Sehemu yake Mwenyewe. Yule aliye
mng'ao wa utukufu wake Baba alikuja katika ulimwengu huu ulionyauka na kuharibika
vibaya kwa laana, na katika tabia yake ya Uungu, yaani, katika mwili wake wa mbinguni,
akaliziba shimo hilo kubwa.... Madirisha ya mbinguni yakafunguliwa na manyunyu ya
neema ya mbinguni yakadondoka katika ulimwengu wetu wenye giza kama vijito vya
uponyaji....
Mungu angekuwa ameitoa [neema yake] pungufu, sisi tusingaliweza kuokolewa. Lakini
Yeye alitoa kwa ulimwengu wetu [neema yake] kwa wingi mno hata isingeweza
kusemwa kwamba angetupenda zaidi [ya vile alivyotupenda]. Basi ni upumbavu ulioje
kwa msimamo ule uliochukuliwa [na watu fulani] kwamba kutakuwa na nafasi ya pili
(second probation) baada ya ile ya kwanza kuisha kabisa. Mungu ametoa wema wake
wote... kwa kuimwaga mbingu yote kwa ajili ya mwanadamu katika kipawa hicho kimoja
kikuu [Yesu Kristo]. Ni kwa kuitambua thamani ya kafara [toleo] hii tu tunaweza
kumfahamu Mungu. Ni upana na kimo na kina kilioje cha upendo wake Mungu! Ni nani
miongoni mwa wanadamu wasiodumu milele awezaye kuufahamu?...
Mungu anamdai mwanadamu ampe mapenzi yake yote, moyo wake wote, roho yake
yote, akili yake yote, na nguvu zake zote. Anatoa madai yake kwa mtu mzima kama
alivyo, kwa sababu amemwaga hazina yake yote ya mbinguni kwa kutupa sisi vyote kwa
wakati mmoja, asibakize kitu cho chote kikubwa kuliko kile mbingu inachoweza
kufanya....
Ninapoanza kuandika juu ya somo hili, huwa naendelea tu kuandika, na kujaribu kuupita
ukingo wake wa nje, lakini nashindwa. Tutakapofika kwenye makao yale juu, Yesu
Mwenyewe atawaongoza wale waliovikwa mavazi meupe yaliyofuliwa na kufanywa
meupe katika damu ya Mwana-Kondoo mpaka atakapowafikisha kwa Baba yake. "Kwa
hiyo wako mbele ye kiti cha enzi cha Mungu, nao wanamtumikia mchana na usiku katika
hekalu lake, na Yeye aketiye katika kiti cha enzi atatanda hema yake juu yao." Ufunuo
7:15. ----- Letter 36a, 1890.

Comments

Popular posts from this blog

Kanuni za kuishi na Watu / Binadam Vizuri

SAIKOLOJIA : PATA KUFAHAMU MAKUNDI MANNE YA TABIA ZA BINADAMU.

Chanzo cha saratani ya matiti