Mojawapo ya mambo muhimu katika mafanikio ya aina yoyote maishani ni kupata msaada wa aina Fulani kutoka kwa watu wengine. Mtu hawezi kufanikiwa bila msaada wa watu,kwa maana hakuna mtu anayejua kila kitu/jambo na anayeweza kufanya kila kitu Duniani. Kwa namna yeyote ile mtu anahitaji msaada wa wengine. Hivyo ili kupata msaada wa wengine ni lazima kujua namna ya kuishi na watu vizuri.Ingawa siyo rahisi kumpendeza kila mtu, lakini watu wengi utaishi nao kwa amani. Zifuatazo ni KANUNI na MBINU mhimu za kuishi na watu vizuri. 1: Uwe na tabia ya kupenda watu kwa moyo wote,hali kadhalika na wewe watakupenda. 2: Heshimu kila mtu na kila mtu umwone ni muhimu sana na wa maana. 3: Usimdharau mtu yeyote kutokana na hali yake,hata akiwa ni masikini ,hakuelimika,hana cheo cha juu na kadhalika. 4: Uwe mtu wa furaha na tabasamu unapokutana na watu. 5: Uwe mcheshi na mtu ambaye watu wanafurahi kuwa nawe. 6: Usipende kulaumu watu na kama utalaumu mtu,tumia njia nzuri na ya up...
Leo nataka tuangalie kilimo cha matikiti kibiashara kwa mtaji wa shilingi laki moja tu(100,000/=). Nimeona niandae hili somo kwa kuwa watu wengi hulalamika kuhusu mtaji lakini kwa asilimia kubwa watu humililiki zaidi ya hii pesa laki moja, lakini bado utamkuta analalamika kuhusu mtaji wa kuanzia. Leo tutaangalia mchanganuo wa shilingi laki moja ili ikuletee milioni moja na nusu(1,500,000/=) kwa makadilio ya chini kabisa hayo ni baada ya siku 75-90 na unaweza pata zaidi ya hapo, ikiwa utaweka juhudi nyingi katika kilimo ambacho unaenda kufanya. Hapa tutaangalia mchanganuo kwa kutumia mbegu bora ya matikiti aina ya PATO F1. Na eneo linalohitajika ni chini ya robo ekari (yaani nusu ya robo ekari ) ila katika laki moja sijaweka gharama ya shamba ambayo ni nusu ya robo ekari yaani mita 500 za mraba. Maandalizi ya shamba. Andaa shamba lenye ukubwa wa mita 500 za mraba( 50m×10m). Baada ya kuliandaa shamba lako hakikisha una mbolea ya kuku ya kutosha mashimo 500 tu na uhakikishe hiyo mbolea...
Hakuna kitu kingine kizuri kama mwili wa mwanamke kwakuwa unaweza kuleta kiumbe binadamu kingine. Mwili wa mwanamke unazo ovari ambazo hutengeneza mayai na homoni maalumu ambazo hudhibiti mwili wake wakati wa ujauzito kuanzia wakati yai linaporutubishwa mpaka mwishoni mwa wastani wa miezi tisa (wakati wa kujifunguwa). Mfumo huu maalumu huanza kazi mara mwanamke anapoanza mzunguko wake wa uzazi (mzunguko wa hedhi). Kwa wastani kila siku 30 ovari zake zitazarisha yai na kuliweka katika mfumo wake wa uzazi likisubiri kurutubishwa. Wakati yai hili limetolewa, mwili wake utaanza kujiandaa kwa uwezekano wa kupata mtoto. Mfuko wa uzazi (uterus) utaanza kubadili uundwaji wake wa seli kwa kuandaa uwezekano wa kukishikilia kijusi (fetus) baada ya yai kurutubishwa. Wakati yai litakapokuwa limerutubishwa ovari zake (mwanamke) zitachukuwa majukumu ya mwili wake na kuhakikisha kuwa kijusi kinapata kile kinachokihitaji ili kuishi. Ubongo wa mwanamke pia huathiriwa kutokana na kutolewa kwa homoni ...
Comments
Post a Comment